Thursday 1 November 2018

AINA ZA WASOMAJI MATINI (TEXT)

Wapo wasomaji wa aina nne (4) katika usomaji wa matini. Wasomaji hao ni: Kenge, Nyoka, Kinyonga na Kobe.
  1. Msomaji Kenge: msomaji huyu ni mkurupukaji mkubwa kwani husoma matini kwa kasi kubwa bila kuzingatia alama za uandishi wala kutafakari maudhui ya matini husika. Ni rahisi sana kuingiza maneno yake mwenyewe.
  2. Msomaji Nyoka: msomaji huyu husoma kwa madaha na mbwembwe nyingi bila kuzingatia maana na mantiki ya kila neno katika matini. Matokeo yake hupotosha kwa urahisi maudhui ya matini.
  3. Msomaji Kinyonga: huyu ni msomaji mzuri sana, si mvivu wa kurudia kusoma tena na tena kwa lengo la kutafakari zaidi. Hata hivyo katika usomaji wake ni rahisi sana kutekwa na hisia za mwandishi. Mara nyingi hubadilisha badilisha maneno na maudhui kutokana na hisia, vionjo na mihemko wakati wa usomaji.
  4. Msomaji Kobe: huyu ni msomaji makini na hana papara, ni mwaminifu katika huzingatia alama zote za uandishi. Daima hutafakari kila akisomacho tena hushirikisha milango yake ya ufahamu.

AMRI KUMI ZA USHAIRI

AMRI KUMI ZA USHAIRI
  1. Ushairi ndiye mungu wako katika shida na katika raha, hakuna mbadala.
  2. Usitunge shairi bure; pasina haja yoyote wala tija.
  3. Shika utakatifu wa ushairi (tunga tungo zenye heshima na taadhima).

Sunday 12 August 2018

SHAHNAM FERDOWSI



Mchango wa Shahnam Ferdowsi katika Ushairi wa Kiswahili

Eric F. Ndumbaro
Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge
Ikisiri
Shahnam (Kitabu cha Wafalme) ni utendi mrefu duniani ulioandikwa katika karne ya 5 na mshairi maarufu wa Kiajemi Hakim Abul-Qasim Mansur (940-1020Ad) ambaye baadaye alijulikana kama Ferdowsi Tusi. Utendi huu umepewa hadhi ya kitaifa na kuwa utendi wa taifa la Iran kutokana na maudhui yake. Shahnama ni utendi unaoelezea historia ya kale tangu kuumbwa kwa ulimwengu, historia ya Dola ya Uajemi mpaka kuingia kwa utawala wa Kiislam katika karne ya 7. Utenzi huu ni mojawapo ya kazi zinazonasibishwa na fasihi ya upinzani. Fasihi ya upinzani ni muundo fasihi unaojipambanua kwa kuonesha upinzani wa watu dhidi ya maadui, wanyang’anyi, wavamizi au wageni. Hata hivyo, fasihi hii haijitanabaishi na kipindi chochote au taifa fulani na imechipuka kutokana na historia ya mwanadamu. (Taheri na Kafi, 2017). Matamanio na malengo ya mwandhishi au mshairi yaliyofichika ndani mwake hujitokeza katika hali ya mtonesho na kudhihirisha uhusiano wake na ung’amuzi na jinsi gani unahusiana na kazi zake za sanaa. Kwa mantiki hiyo ukinzani wa kitafaifa unaojitokeza katika kazi mbalimbali za washairi ni matokeo ya mfifizo wa hapo awali. Utafiti huu una lengo la kuchunguza mashairi ya Kahigi kama yana mhamisho wowote wa mtonesho unaodhihirisha vipengele/elementi zozote zinazoashiria uendelevu wa Shahnameh Ferdowsi kama miongoni mwa fasihi kinza katika ushairi wa Kiswahili.

WASHAIRI CHIPUKIZI


Malenga Chipukizi wa Karne ya 21 katika Utungaji wa Mashairi Bora: Changamoto na Masuluhisho yake



Neema B. Sway
Taasisi ya Taaluma za Kiswahili, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
&
Eric F. Ndumbaro
Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mwenge


Hali ya malenga wa Kiswahili katika miaka ya 1960 hadi 1990 ilikuwa tofauti sana katika suala la usukaji wao wa mashairi kifani na kimaudhui ikilinganishwa na wa miaka ya 2000 hasa katika kizazi cha karne hii ya sayansi na teknolojia. Katika miaka ya 1960, washairi wengi walitunga tungo zenye viwango vinavyokidhi jamii zao kiasi cha kuacha mwangwi usiofifia hata katika vipindi vilivyofuata. Mafanikio haya pengine yalifikiwa kutokana na sheria walizojiwekea ambazo ziliwaongoza katika utungaji wao wa mashairi. Kwa upande wao, malenga chipukizi wa karne hii, wanakabiliwa na changamoto nyingi ambazo zinawafanya kutunga tungo chapwa na zenye wepesi wa fani na mawanda ya kimaudhui. Je, ni changamoto gani zinazowafanya malenga chipukizi wa karne ya 21 kushindwa kupea katika kutunga tungo za Kiswahili zenye ladha, uzito, mvuto na ubora unaostahili? Je, ni masuluhisho yapi yatakayoweza kusaidia katika kukabiliana na changamoto hii inayowasonga malenga chipukizi wa karne ya 21? Hivyo basi utafiti huu unalenga kuchunguza changamoto zinazowakabili malenga chipukizi wa Kiswahili wa karne ya 21 na kupendekeza masuluhisho ili kufikia utungaji wa mashairi bora ya Kiswahili. Utafiti huu umekusanya data zake kwa njia ya usomaji wa maandiko mbalimbali ya kifasihi na kinadharia na majadiliano na wapenzi wa mashairi kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii. Makala hii inatarajia kuchochea ubunifu wa uandishi wa mashairi kifani na kimaudhui kwa malenga chipukizi wa Kiswahili. Aidha, utafiti huu utahamasisha tungo zenye ladha, mvuto na ubora unaostahili kwa malenga chipukizi.

Thursday 10 March 2016

Semantiki na Taaluma nyingine



UHUSIANO WA SEMANTIKI NA TAALUMA NYINGINE
Makala haya yatashughulikia semantiki na taaluma zingine zinazokaribiana nazo kama semiolojia, leksikolojia, leksikografia na pragmantiki kwa kuangalia ufanano na utofauti wake na mwisho hitimisho.
Semantiki ni taaluma katika isimu ambayo hushughulikia maana ya maumbo au sentensi katika lugha. Taaluma hii ilianza enzi za Aristotle na Plato ambao walizingatia zaidi sifa za maana, katika kipindi hicho walitaka kujua sifa na tabia za maana. Leech (1981) anasema

Ugumu wa Kufasili Neno



NI VIGUMU KUFASILI MAANA YA NENO KIKAMILIFU”
Kazi hii itaonesha namna kulivyo na ugumu wa kufasili neno. Pia itaeleza kiini cha ugumu huo wa kufasili neno kikamilifu kwa kuzingatia fasili za wataalamu mbalimbali wa isimu.
TUKI (2004) wanadai kuwa neno kama kipashio cha usemaji ambacho hujengwa na mwanadamu au mkururo wa sauti zilizopangika kisilabi na ambazo hutambuliwa na wasemaji wa lugha inahusika kuwa kitu kimoja chenye maana mahususi. Naye Mdee (2010:5) anafasili neno kwamba ni mfululizo wa herufi ulioafungamana pamoja na kuzungukwa na nafasi tupu. Pia Kihore na wenzake (2001) wanafasili neno kwa kutulia maanani maelezo ya Lyons (1984:194-208) kuwa neno linaweza kufafanuliwa katika misingi ya kiumbo-sauti (yaani, kwa kuchunguza sauti zinazounda umbo zima), kiotografia (yaani kwa kuchunguza herufi zinazotumika katika kuliundika umbo lake) na kisarufi (yaani, kwa kuchunguza kilekinachowakilishwa na umbo husika katika lugha)

Sunday 6 March 2016

TENDI TATU ZA KALE



UCHAMBUZI WA TENDI TATU ZA KALE 

Ikisiri
Tangu Finnegan (1970:108) alipodai kwamba, katika fasihi simulizi ya Afrika Kusini mwa Sahara ni nadra sana kupata Tendi, dai hili limeibua mjadala mrefu wa kitaaluma miongoni mwa wataalam mbalimbali wakiwamo: John William, Thomas A. Hale na Stephen Belcher ambao ndio waliodondoa baadhi ya beti katika tendi za Kiafrika na kuziweka pamoja katika kitabu kinachojulikana kwa jina la Oral Epic from Africa: Vibrant Voices from a Vast Continent. Mbali na hao, mtaalam mwingine ni Mulokozi (1999) ambaye naye anathibitisha upo wa tendi katika Afrika Mashariki kwa kukusanya pamoja tenzi tatu za kale katika kitabu cha Tenzi Tatu za Kale. Pia kuna mtaalamu mwigine Belcher (1999) ambaye naye alizungumzia tendi za Kiafrika katika kitabu chake kinachojulikana kwa jina la Epic Tradition of Afrika. Hivyo basi, ni wazi kwamba uchapishaji wa vitabu hivi ni matokeo chanya ya tafiti zilizofanywa na wataalamu mbalimbali na kuamua kukusanya na kuziweka pamoja kama mifano ya uwakilishi wa utamaduni wa tendi Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kwa lengo la kufungua milango ya kutambulika zaidi.
1.0     Utangulizi
Makala hii itajishughulisha zaidi na mapitio-hakiki ya vitabu viwili ambavyo ni, Oral Epic from Africa: Vibrant Voices from a Vast Continent na Tenzi Tatu za Kale. Katika mapitio hayo vipengele mbalimbali vitajadiliwa kama vile: fasili ya tendi, mpangilio wa tendi katika vitabu hivyo, waandishi wa vitabu husika, uhakiki: usuli wa yeli/manju, usuli wa kijamii-kihistoria, utendaji-uwasilishwaji, udhaifu/mapungufu, ubora wa kazi, ulinganisho na tendi nyingine, hitimisho na marejeo. Kwa kuanza na fasili ya tendi;

Tuesday 29 December 2015

Tasnifu



UFUNDISHAJI WA NADHARIA ZA UHAKIKI WA FASIHI YA KISWAHILI KATIKA TANZANIA
FURAHA J. MASATU
SHAHADA YA UZAMILI KATIKA FASIHI YA KISWAHILI
CHUO KIKUU CHA DODOMA
JUNI 2011
UFUNDISHAJI WA NADHARIA ZA UHAKIKI WA FASIHI YA KISWAHILI KATIKA TANZANIA
Furaha J. Masatu

Monday 14 December 2015

SAIKLOPEDIA NA KAMUSI


TOFAUTI BAINA YA SAIKLOPEDIA NA KAMUSI
Kamusi na Saiklopidia ni dhana mbili zenye mkanganyiko mkubwa hasa katika suala zima la maana na matumizi. Aidha wataalam mbalimbali wametoa fasili ya dhana hizi ili kuweka bayana tofauti zilizopo baina ya Saiklopidia na Kamusi.

KAMUSI


UCHOMOZAJI WA KAMUSI ZA AWALI KATIKA BARA LA ULAYA NA MAENDELEO YALIYOFIKIWA KATIKA KARNE HII
 (Eric Ndumbaro)
1.0  IKISIRI
Katika jamii yoyote ile ulimwenguni dhana ya maendeleo haiji kama mvua, bali huanza hatua kwa hatua. Hali kadhalika hatua hizo hujibainisha katika historia kwa kupitia vipindi mbalimbali jamii tangu jamii ilipoanza kujikongoja katika masuala mbalimbali mpaka hivi sana na hata kubashiri mwelekeo wa jamii katika nyakati zijazo. Hivi ndivyo hata taaluma ya leksikografia ilivyoanza na hatimaye uchomozaji wa kamusi za awali katika bara la Ulaya mpaka kufikia maendele tuliyonayo katika karne hii.

Monday 26 October 2015

SHAIRI


SINA DOGO!

Wapendwa sikilizeni,
Uchoyo si jadi yangu,
Nilosikia jamani,
Mlijue na wenzangu,
Mimi daima napenda,
Kuwajuza wasujua,
Tena hata kuwafunda,
Ili wasije shupaa,

Thursday 17 September 2015

TANZU ZA FASIHI SIMULIZI



Tanzu na Vipera Vya Fasihi Simulizi

Kwa mujibu wa Mulokozi katika Mulika namba 21(1989). Pamoja na kwamba Fasihi ni kongwe lakini kitaaluma bado ni changa kwa sababu ilianza kuchungunzwa hivi karibuni. Hivyo imepelekea kutokuwepo kwa nadharia, marejeo, wala istilahi zenye kutosheleza mahitaji ya taaluma hiyo. Tatizo hili linadhihirika pale tunapoangalia kazi za wataalamu mbalimbali kuhusu tanzu za Fasihi Simulizi.
Kwa upande wa nadharia kitabu pekee kinachozijadili tanzu za Fasihi Simulizi kwa urefu ni kitabu cha Ruth Fennegan kinachoitwa Oral Literature in Africa (1970). Kwa upande wa Kiswahili hakuna kitabu kinachojadili uwanja wa tanzu za Fasihi Simulizi. Badala yake

FONOLOJIA

Fonolojia Ya Kiswahili
Neno fonolojia linatokana na maneno mawili ya Kigiriki phone-sauti za kusemwa na logos- taaluma/mtalaa. Masimulizi yanadai kuwa taaluma hii ilianza zamani sana kati ya mwaka 460 kabla ya Masihia huko India ya kale, ambapo mtu aliyeitwa Panini, na ambaye huaminika kuwa ni baba wa isimu aliandika kuhusu fonolojia ya Kisansikriti katika matini aliyoiita Shiva Sutras. Ni katika andiko hili ndipo alipobainisha kuwepo kwa dhana ambazo leo hii hujulikana kama fonimu, mofimu na mzizi.
Baada ya andiko hilo, habari za taaluma ya fonolojia ni kama zilipotea kabisa katika uwanja wa isimu hadi ilipofika karne ya 19 ambapo wanaisimu wengine waliibuka na kuzungumzia upya masuala ya fonolojia. Miongoni mwa wanaisimu wa mwanzo wanaotajwa

Sunday 14 June 2015

NGANO



SIFA YA NGANO NI UFUPI PAMOJA NA MUUNDO WA MOJA KWA MOJA. JADILI
Katika kujibu swali hili kwanza itaelezwa maana ya ngano kwa mujibu wa wataalamu mbalimbali, kisha kiini cha swali na mwisho litatolewa hitimisho ambapo tutatoa mapendekezo kuhusu maana ya ngano
Kwa kuanza na maana ya ngano, Hamisi na Madumulla (1989:5) wanaeleza kuwa

Tuesday 16 December 2014

SHAABA ROBERT

MAANDIKO YA SHAABAN ROBERT

Kwa mujibu wa waandishi na watafiti mbalimbali, mfano Sengo (1975), Kezilahabi (1976) na Gibbe (1980) wanasema kuwa jumla ya kazi alizowahi kuzitunga Marehemu Sheikh Shaaban Robert na zilizochapishwa hadi sasa ni ishirini na mbili, ambapo kumi na nne ni za ushairi na nane ni za nathari. Hata hivyo baadhi ya maandiko ya watafiti wa hivi karibuni mfano Mulokozi (2002) na Chuachua (2008) yanaonesha kuwa jumla ya maandiko ya Sheikh Shaaban Robert yaliyokwisha kuchapwa hadi hivi sasa ni ishirini na nne.
Ponera (2010) anaungana na Mulokozi (2002) na Chuachua (2008) kwa kuorodhesha vitabu ishirini na nne vya Sheikh Shaaban Robert vikiwa kumi na nne ni vya ushairi na kumi ni vya nathari.
Ponera (2010) anavitaja vitabu hivyo vya ushairi kuwa ni:
1) MWAFRIKA AIMBA (1969), Nelson. Nairobi
2) ALMASI ZA AFRIKA (1971), Nelson, Nairobi
3) KOJA LA LUGHA (1969), Oxford, Nairobi
4) INSHA NA MASHAIRI (1967), Nelson, Nairobi
5) ASHIKI KITABU HIKI (1968), Nelson, Nairobi
6) PAMBO LA LUGHA (1968), Oxford, Nairobi
7) KIELEZO CHA FASILI (1962), Nelson, Nairobi
8) MASOMO YENYE ADILI (1959), Art&Literature, Nairobi
9) MAPENZI BORA (1969), Nelson, Nairobi
10) TENZI ZA MARUDI MEMA NA OMAR KHAYYAM (1973), TPH, Dar-es- salaam
11) UTENZI WA VITA VYA UHURU (1961), Oxford, Nairobi
12) ALMASI ZA AFRIKA NA TAFSIRI YA KIINGEREZA (1960), Art&Literature, Nairobi
13) MASHAIRI YA SHAABAN ROBERT (1971), Nelson, Nairobi
14) SANAA YA USHAIRI (1972), Nelson, Nairobi.
Na vitabu vya nathari vya Sheikh Shaaban Robert ni:
15) KUFIKIRIKA (1968),Oxford, Nairobi
16) WASIFU WA SITI BINTI SAAD (1967), Art&Literature, Nairobi
17) MAISHA YANGU NA BAADA YA MIAKA HAMSINI (1949), Nelson, Nairobi
18) KUSADIKIKA (1951), Nelson, Nairobi
19) ADILI NA NDUGUZE (1977), TPH, Dar-es- salaam
20) UTU BORA MKULIMA (1968), Nelson, Nairobi
21) SIKU YA WATENZI WOTE (1968), Nelson, Nairobi
22) KIELELEZO CHA INSHA (1954), Witwatersand, Nairobi
23) BARUA ZA SHAABAN ROBERT 1931- 1958, (2002), TUKI, Dar- es- salaam 24) MITHALI NA MIFANO YA KISWAHILI (2007), TUKI, Dar-es- salaam.
MAREJELEO
Sengo,T. S. Y (1973), SHAABAN ROBERT: UHAKIKI WA MAANDISHI YAKE. Longman; Dsm
Kezilahabi, E (1976), USHAIRI WA SHAABAN ROBERT. EALB Nairobi
Gibbe, A. G (1980), SHAABAN ROBERT; MSHAIRI.TPH. Dsm
Mulokozi, M. M (2002) BARUA ZA SHAABAN ROBERT 1931-1958. TUKI. Dsm
Chuachua, R (2009) NAFASI YA MWANAMKE KATIKA NATHARI ZA SHAABAN ROBERT: Ripoti ya Utafiti Chuo Kikuu cha Waislam (Haijachapwa)
Ponera, A (2010) ATHARI ZA UFUTUHI KATIKA NATHARI ZA SHAABAN ROBERT Tasnifu ya Uzamili Chuo Kikuu cha Dodoma
……………………………….

Monday 13 October 2014

KIAMBISHI TAMATI "NI"



KIAMBISHI TAMATI “NI”
Makala haya yatashughulikia ufupisho wa makala ya Swahili forum iliyohaririwa na rose – marie beck, Thomas gelder na wemer graefner katika uchambuzi wa kiambishi tamati cha mahali –ni, tathmini na mwisho hitimisho.
Makala haya yanahusu asili na usambaaji wa kiambishi tamati cha mahali –ni. Karibu  lugha zote za kibantu kuna ngeli tatu za mahali zenye viambishi pa, ku, mu, kwa mfano katika lugha ya kisangu viambishi hivi vya mahali  hujitokeza pia katika maneno ya mu-khati, pa-khati, na ku-khati. Kwa upande wa lugha ya kiswahili mofimu hizi yaani pa, ku, mu hutumika kama viwakilishi vionyeshi kwa mfano hapa, huku na humu na vilevile hufanya kazi kama viwakilishi  vimilikishi. Kwa mfano  kwetu, kwao na mwao. Dai hili limetolewa na Beck na wenzake (1994). Swali la msingi, kama viambishi vya mahali vinavyojitokeza katika ngeli hizo, kiambishi –ni- hakipo, kiambishi hiki kimetoka wapi?

uMarx



UHAKIKI WA kiMarx
Karl Marx (1818-83) na Friedrich Engels (1820-95
  -Hawa ndio waasisi wa mtazamo huu. Hata hivyo wao wenyewe hawakuandika sana kuhusiana na fasihi.
·         Hoja tatu Muhimu
  • 1.      Katika historia ya mwanadamu, jamii na mahusiano yake, taasisi zake namna yake ya kufikiria; mambo yote hayo hutegemea mabadiliko ya mfumo wa uzalishaji mali. Yaani jinsi uchumi, uzalishaji, mgawanyo na umilikaji mali unavyoendeshwa
2.      Mabadiliko ya kihistoria katika msingi wa uzalishaji mali yanaathiri mabadiliko ya muundo wa matabaka ya jamii, na hivyo kutokeza (kwa kila wakati) tabaka tawala na tawaliwa ambayo huwamo katika mapambano na harakati za kugombea uchumi, siasa na faida za kijamii. 
3.      Urazini wa mwanadamu umeundwa na itikadi, Imani, thamani ya kitu (value), na namna za kufikiri na kuhisi
·   Ni kupitia katika hivi, mwanadamu huuona ulimwengu wake, na huelezea yale yaliyomzunguka na yale anayoyaona kuwa ukweli.
ATHARI KATIKA FASIHI
Waandishi wa Ki-Marx huandika kwa kutumia falsafa ya Ki-Marx na jinsi alivyoiona historia ambapo wazo kuu ni kuwa: harakati za matabaka ndio msingi mkuu unaofanya mambo yawe kama yalivyo.
Nguvu ya Historia
Jinsi gani wanavyoweza kuufahamu ulimwengu uliopita kwa kutumia vielelezo na uthibitisho wa kihistoria.
Mfano:  Matini km. Riwaya inawakilishaje ukweli? Ukweli huo ni usahihi wa mambo ktk Jamii. Usanii ni uumbaji wa Ukweli ktk maisha?
UHALISIA WA KISOSHALISTI
Mwandishi au msanii yeyote, ajitoe kuandika na kulielimisha kuhusu tabaka la wafanyakazi. Na kwamba, fasihi ni lazima iwe ya kimaendeleo, na ioneshe mtazamo wa kimaendeleo katika jamii
Georg Lukács (1885-1971) Hungary
Nadharia yake: Kiakisiko
Kwamba mambo yote huakisi ukweli fulani wa maisha. Kazi ya fasihi huakisi mfumo fulani unaofumbuka polepole. Kutuonesha mivutano, mikizano na au migogoro iliyomo katika maisha ya jamii inayoakisiwa.
KIAKISIKO
Kilicho cha msingi ni maudhui na sio fani yake. Fani inachukua nafasi ndogo sana katika kazi ya fasihi.
Mgogoro wa Ushairi wa Kiswahili.
Brecht alipingana naye kwa kusema hatuwezi kushikilia sheria za sanaa katika muda wote kwani ukweli wa jamii hubadilika.
MKABALA WA FRANKFURT 1923-1950
Nadharia Hakiki
Theodor Adorno, Max Horkheimer na Herbert Marcuse.