Sunday 22 September 2013

SINTAKSIA



MIKABALA YA TAALUMA YA SARUFI.
(a)          Sarufi ubongo
(b)          Sarufi kama kaida za kiisimu.
(c)    Sarufi kama tafiti na uchambuzi wa miundo inavyooneka kwenye lugha.
UTANGULIZI WETU UTAZINGATIA MAMBO YAFUATAYO
·        Maana ya sarufi.
·        Mkabala wa kimapokeo.
·        Mkabala wa kisasa.

ASILI YA KISWAHILI



ASILI YA KISWAHILI: FREEMAN GENVILLE KATIKA “MEDIEVAL EVIDENCES FOR SWAHILI”
Kwanza tutaangalia nini maana ya neno asili, pia tutaeleza kwa ufupi mitazamo mbalimbali kuhusu asili ya lugha ya Kiswahili, halafu tutaangalia kwa undani kiini cha mada yetu kwa kuchanganua vyema mawazo ya Freeman Grenville katika makala yake inayoitwa ‘Medieval Evidences for Swahili’ pia tutaonesha ubora pamoja na udhaifu wake na mwisho tutatoa hitimisho.
Neno asili kwa mujibu wa Massamba na wenzake (1999:3) ni jinsi kitu au jambo lilivyotokea au lilivyoanza.  Fasili hii ni nzuri na inajitosheleza kwa maana kwamba jambo au kitu kinaweza kutokea kibahati kama ilivyo katika lugha au linaweza kuanzishwa.

Friday 20 September 2013

CHIMBUKO - USHAIRI



CHIMBUKO LA USHAIRI
Dhana ya ushairi imejadiliwa na wataalamu mbalimbali huku kila mmoja akitoa fasili yake. Baadhi ya wataalam hao ni kama ifuatavyo:
Mssamba, (2003) akimnukuu Shaban Robert, anasema; “ushairi ni sanaa ya vina inayopambanuliwa kama nyimbo, mashairi na tenzi zaidi ya kuwa na sanaa ya vina ushairi unaufasaha wa maneno machache au muhtasari.”
Mnyampala (1970) anasema kuwa “ushairi ni msingi wa maneno ya hekima tangu kale ndicho kitu kilichobora sana maongozo ya Dunia kwa kutumia maneno ya mkato na lugha nzito yenye kunata iliyopangwa kwa urari wa mizani na vina maalum.”
Amri Abeid (1954:1) anasema kuwa “ushairi au utenzi ni wimbo, hivyo kama shairi haliimbiki halina maana.”

USHAIRI



DHANA  NA DHIMA  YA USHAIRI WA KISWAHILI
Kwa mujibu Mulokozi (1996) anasema, wataalamu wengi wamekubaliana kuwa asili ya ushairi wa Kiswahili ni tungo simulizi, hasa ngoma na nyimbo zinazofungamana na ngoma.
Kabla ya karne ya 10 BK ushairi wa Kiswahili ulikuwa ukitungwa na kughanwa  kwa ghibu bila kuandikwa.  Wataalamu hao waliojadili historia ya ushairi ni kama (Chiraghdin 1971: 7:10, Massir 1977:1 Ohly 1985:467).
Dhana ya ushairi imejadiliwa kwa kuangalia makundi mawili ya waandishi wa mashairi ya Kiswahili, makundi hayo ni kundi la wanamapokeo, na kundi la wanausasa.
Tukianza na kundi la wanamapokeo.  Wataalamu mbalimbali wamejadili dhana ya ushairi kama ifuatavyo:

Friday 13 September 2013

ISIMUJAMII



“ISIMUJAMII NA ISIMU KAMA TAALUMA MBILI, HUTOFAUTIANA LAKINI KIMSINGI HUKAMILISHANA.”
Taaluma ya isimujamii ilianza huko Marekani katika miaka ya 50 na 60. Ilianza na wanasosiolojia kama vile Fishman (1971) na wanaanthropolojia kama vile Del Hymes (1972) na wengine ni wanaisimu kama vile akina Labov William (1972), Gumperz (1972) na Bright William (1965). Wataalamu hawa walitaka kujua tofauti za tamaduni ngeni huko Marekani ambapo kulikuwepo na wamarekani wenye asili ya kiafrika na wamarekani wahindi (wahindi wekundu). Hivyo walitaka kuzifahamu tamaduni hizo ngeni ili waweze kuzifanyia kazi katika elimu. Na hapo ndipo isimujamii ilipoanza Mekacha (2000).
Katika kufasili isimujamii Msanjila na wenzake (2011) wanasema kwamba, wataalamu mbalimbali wa lugha wanakubaliana kimsingi kwamba isimujamii ni taaluma inayoshughulika na uchunguzi unaolenga kufafanua uhusiano uliopo kati ya isimu na jamii. (kwa mfano Trudgill 1983; Hudson 1985 na Mekacha 2000).

UAMILIAJI LUGHA


TOFAUTI KATI YA UAMILIAJI LUGHA NA UJIFUNZAJI LUGHA.
Mwanadamu anapozaliwa anakuwa na bohari la sauti mbalimbali zisizo na maana yoyote, na mara anapoanza kuishi katika jamii ndipo huanza kuibua sauti hizo katika mazingira ya kinasibu (pasipo yeye mwenyewe kutarajia) na kuanza kuzitafutia maana sauti hizo. Uibuaji wa sauti hizo huendana sambamba na mambo yanayomzunguka pamoja na yale anayoyatumia.
Hii tunaona hata kwa watoto wachanga jinsi wanavyoanza kuongea, kwanza huanza kwa kutoa sauti zisizo na maana yoyote kisha kadiridi wanavyokuwa ndivyo sauti hizo zinaanza kubadilika mpaka zikaeleweka na watu wanaomzunguka. Yote haya ufanyika kutokana na msaada wa mazingira, muda pamoja na jamii inayomzunguka.

FASIHI YA WATOTO NA VIJANA



NI VIGUMU KUWEKA MIPAKA DHAHIRI KATI YA FASIHI YA WATOTO NA VIJANA NA YA WATU WAZIMA.
Ni vyema kuanza kufafanua maana za maneno mbalimbali ya msingi yaliyojitokeza katika kauli hii kama vile: maana ya fasihi kwa ujumala, maana ya fasihi ya watoto na vijana, maana ya fasihi ya watu wazima pamoja na maana ya mipaka. Baada ya hapo kiini cha mada, ambapo tutaona ukubalifu wa hoja, kisha zitafuata sababu zinazoonesha ugumu wa kuweka mipaka dhahiri kati ya fasihi ya watoto na vijana na ya watu wazima.
Mulokozi (1996) anafafanua kuwa fasihi ni sanaa ya lugha inayoangalia maisha na mazingira halisi ya mwanadamu kwa kutumia lugha na maandishi
Kwa mujibu wa Ngure (2003:1) fasihi ni aina ya sanaa ambayo wasanii wake huonesha ustadi wao katika kutumia maneno kisanaa ili kuwasilisha ujumbe wao kwa wasomaji/jamii iliyonuiwa.

Sunday 8 September 2013

FASIHI ANDISHI YA KISWAHILI



HADHI NA NAFASI YA FASIHI ANDISHI YA KISWAHILI KITAIFA NA KIULIMWENGU.
(Eric Ndumbaro – UDSM)




Utangulizi
Kadri jamii inavyobadilika ndivyo na historia inavyobadilika. Yote haya yanakwenda katika usambamba sawia. Hivyo kilichopo leo kinaweza kuwa sawa au tofauti na cha jana na ukweli wa jana waweza kuwa ukweli au uongo wa leo au kesho, kwa maana hiyo jamii na historia yake si tuli (static).