DHANA NA DHIMA
YA USHAIRI WA KISWAHILI
Kwa
mujibu Mulokozi (1996) anasema,
wataalamu wengi wamekubaliana kuwa asili ya ushairi wa Kiswahili ni tungo
simulizi, hasa ngoma na nyimbo zinazofungamana na ngoma.
Kabla ya karne ya 10 BK ushairi wa Kiswahili
ulikuwa ukitungwa na kughanwa kwa ghibu
bila kuandikwa. Wataalamu hao
waliojadili historia ya ushairi ni kama (Chiraghdin 1971: 7:10, Massir 1977:1
Ohly 1985:467).
Dhana ya ushairi imejadiliwa kwa kuangalia makundi
mawili ya waandishi wa mashairi ya Kiswahili, makundi hayo ni kundi la
wanamapokeo, na kundi la wanausasa.
Tukianza na kundi la wanamapokeo. Wataalamu mbalimbali wamejadili dhana ya
ushairi kama ifuatavyo: