Thursday 28 November 2013

SINTAKSIA


Katika kategoria zilizokuwa ndani ya Kiswahili ni neno la kategoria gani huchagua kategoria ipi?
Makala haya yatajadili  maana ya kategoria, yataainisha kategoria mbalimbali za maneno kwa mujibu wa wataalamu, yatajadili kategoria gani huchagua kategoria ipi katika tungo za Kiswahili, yatabainisha sababu zinazopelekea kategoria kuchaguana na kujaribu kuunda kanuni mbalimbali na hatimaye kuhitimisha.
Kategoria za maneno ni aina za maneno kadri ya uainisho wake kutegemeana na sifa za maneno husika kuwekwa katika kundi moja. Mfano Kategoria ya Nomino, Kategoria ya vitenzi, kategoria ya vivumishi.
Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu (2004) maneno yameainishwa katika makundi nane. Makundi hayo ni Nomino, Kitenzi, Kivumishi, Kiwakilishi, Kielezi, Kihusishi, Kihisishi na Kiunganishi. Ambapo kategoria hizi zimepangwa kulingana na sifa za maneno yanayoingia ndani yake.  

Kihore na wenzake (2003) wanaainisha kategoria saba za maneno nazo ni nomino, vitenzi, vivumishi, viwakilishi, viunganishi, vielezi na viingizi.
Kwa pamoja wataalam hawa wanakubaliana kuwepo kwa kategoria za maneno ingawa wanatofutiana katika idadi ya aina za kategoria.Tofauti hizi zinatokana na baadhi ya maneno yanaonekana kutoingia katika kategoria zilizoainishwa. Kwa mfano kategoria ya maneno kama

Wednesday 27 November 2013

UAMILIAJI LUGHA


SARUFI MAJUMUI NA UAMILIAJI LUGHA YA PILI.
Makala haya yataangalia maana ya sarufi majumui, masuala ya msingi yanayohusu maarifa ya lugha, sifa za sarufi majumui, sarufi majumui na uamiliaji lugha ya pili na mwisho tathmini.
Kwa mujibu wa Chomsky (1976:29) kama alivyonukuliwa na Ellis (1996:430) sarufi majumui ni mfumo wa kanuni na sheria ambazo ni msingi wa lugha za binadamu (tafsiri yangu). Muasisi wa nadharia hii ni Noam Chomsky.
Msingi wa nadharia hii ni kwamba binadamu anapozaliwa anakuwa na maarifa asilia ambayo humsaidia katika ujifunzaji lugha; mambo ya ndani na nje ambao husaidia katika uamiliaji wa lugha. Maarifa haya hupatikana pale tu binadamu anapozaliwa kwani huwa na kifaa cha uamiliaji lugha ambacho kinakuwa na kanuni majumui na kanuni badilifu ambazo hukutana na tajiriba (uwezo wa jamii katika lugha) na kusababisha uamiliajli lugha kutokea.

Waamiliaji wa lugha ya kwanza huwa na maarifa asilia ambayo huwawezesha kuiamili lugha yao kwa kutumia maarifa hayo. Hivyo

UTENDI WA SON-JARA


UTENDI WA SON- JARA
Dhana ya utendi katika fasihi ya Kiswahili, iliwahi kuzua utata baada ya Ruth Finnegan (1970) kusema kwamba Afrika hakuna tendi bali kuna simulizi za kisifo. Hoja hii aliipa uzito kutokana kwamba aliangalia tendi andishi na kusahau tendi simulizi. Vilevile vipengele muhimu vya tendi simulizi hakuvipa umuhimu kama vile usimulizi na utendaji. Vigezo muhimu alivyovitaja ni :
(1)Utendi uwe na umbo la kinudhumu.
(2)Urefu.
(3)Uzungumzie maisha ya shujaa.
(4)Muunganiko wa matukio.
Kutokana na vigezo hivyo aliona kwamba kuna tendi zenye sifa hizo, isipokuwa sifa ya nudhumu na tendi hizo ni Son-Jara, Mwendo na Lianja. Madai yake yaliibua wataalamu mbalimbali kufatiti na...

Tuesday 26 November 2013

UFUNDISHAJI LUGHA

UFUPISHO WA SURA YA PILI KATIKA HAMMERLY, H (1982) SYNTHESIS IN SECOND LANGUAGE TEACHING: AN INTRODUCTION TO LINGUISTICS.
LUGHA
Wakati wa vita Waziri Mkuu alikuwa akimalizia hotuba yake bungeni kwa kusema, "Tutakilinda kisiwa chetu kwa gharama yoyote, tutapigana ufukweni, tutapigana nchi kavu, tutapigana milimani, bila kukata tamaa...."Hii ilikuwa ni sehemu ya hotuba iliyotolewa na Winston Churchill tarehe 4.6.1940 bungeni na kuibua ghasia na kila aliyeisikia hataisahau hotuba hii. Mfano huu unaonyesha jinsi lugha inavyojitokeza kuanzia silabi moja mpaka kufikia usemaji wenye ufasaha na kupata waandishi makini.
Lugha ni nini?
Wataalamu mbalimbali wanatofautiana kuhusu maana ya lugha. Kwa karne nyingi wanafalsafa waandishi, wanasaikolojia na wanaisimu wametoa maana mbalimbali za lugha. Tukirejea kwenye Isimu na sayansi ya lugha kuna maana mbalimbali za lugha kama ilivyo Isimu. Kutokana na maana mbalimbali zilizotolewa tunaweza kuwa na maana ya jumla kama ifuatavyo:

Sunday 17 November 2013

HADITHI

       MAJUTO NI MJUKUU  

Hapo zamani za kale, hapa kwetu kijijini,
Kijiji kilo vutia, pande zote za dunia,
Walifurika wageni, maajabu jionea,
Masikini mwananchi, majuto ni mjukuu.

Ardhi yenye madini, mito mbuga za wanyama,
Viumbe wa maajabu, mlima wenye theluji,
Maziwa yalofurika, viumbe kila aina,
Maskini mwananchi, majuto ni mjukuu.


Friday 15 November 2013

SANAA YA USHAIRI


USHAIRI
Shaaban Robert katika uandishi wa ushairi ameandika Tenzi na mashairi ya kimapokeo.
Tenzi: Ni aina ya mashairi ya kimapokeo wenye sifa zifuatazo:
  • Kimaudhui; Ni utungo wenye maudhui yanayosimulia kwa urefu tukio fulani maalum. Waweza kuwa wasifu wa mtu au jambo la kihistoria. Mfano; S. Robert ameandika utenzi wa vita vya Uhuru, ameeleza kuhusu historia. Pia katika Mapenzi Bora, ameeleza kuhusu sifa za mapenzi bora.
  • Utenzi ni utungo wa pili kati tungo za ushairi zenye beti nyingi. Utungo wa kwanza unaoongoza kuwa na beti nyingi kuliko zote katika ushairi ni Tendi. Lakini hapa tutaangazia tenzi zaidi.

Wednesday 13 November 2013

SHAABAN ROBERT


DHANA YA MAPENZI KATIKA KAZI ZA SHAABAN ROBERT
Mapenzi ni hali ya kuingiwa moyoni na kuthamini mtu au kitu zaidi ya mwingine au kingine.
Pia mapenzi ni hali ya kujali jambo, kitu au mtu zaidi ya mwingine. S. Robert amejaribu kufafanua dhana ya mapenzi kama dhana pana sana, anaeleza kuwa:
  • Mapenzi ni hali ya kumpenda Mungu
  • Mapenzi ni yale ya kupendana sisi kwa sisi
  • Mapenzi ni yale yasiyo bagua umri, kabila au kazi, taifa, rangi nk.
  • Mapenzi ni yale yasiyojali tofauti baina ya watu
  • Mapenzi ni ile hali ya kupendana bila kikomo 
  • Mapenzi ni yale ya kuridhika na hali zetu. Mfano; katika kitabu chake cha Mapenzi Bora nk,

KITUSHI


KITUSHI CHA BABU NA MJUKUU
Mjukuu:      Babu hebu nisaidie Mjukuu wako! maana naona maluweluwe. Hivi Babu! kile, vile, hivi na hivyo vilianza vile, hivyo au vilevile na wale je au ndo’ walewale. Maana wengi wanasema eti sawa na sawasawa ni sawasawa!! Napata mkanganyiko. Alafu na wale je? Walianza vile au vilevile kama wale? Mbona nashindwa kuelewa naona uvulivuli tu!! kati ya kile, kilekile, vile, vilevile na hivi, hivihivi na alafu tena eti hivyo na hivyo hivyo! ni sawa lakini si sawasawa!! Hapo Babu ndipo ninaposhaa’ maana kama vile ni vilevile na hivyo ni hivyohivyo na sawa ni sawasawa, sasa kwa nini vile vina kuwa hivyo, au vinakuwa sawasawa? Na kama hivyo ni vile au ni sawa na si sawasawa mbona sisi tuko hivi na si vile? Na kama kweli ni hivi kwa nini wewe unang’ang’ania vile na si hivyo wala hivyohivyo na wala hivi. Au Babu labda kwa sababu ya kale kamsemo kako ka Jembe kwanza?” na kale wimbo kako kenye ubeti mmoja wenye vipande mshororo vitatu vyenye vina vya ukwapi, utao na mwanda!! huku kakiwa na uradidi wa neno moya!! teh!eeeee teheeee! teh!eeee teh! teh! teh! teh!...ha ha haha ha haaa…!!

TAMTHILIA


UANDISHI WA TAMTHILIA
Tamthilia ni nini?
  • Tamthilia ni utanzu ambao hutegemea mazungumzo na uigizaji ili kuwasilisha ujumbe wake. Huu ni utanzu ambao huandikwa kwa mtindo wa mazungumzo ya wahusika (Wamitila, 2007).
  • Nkwera (h.t) anaelezea kuwa tamthilia ni: Tamthilia ni mchezo wa kuigiza au utungo wa kisanaa ambao huweka wazo fulani katika matendo na mazungumzo (Nkwera, h.t)
AINA ZA TAMTHILIA
  • Kwa mujibu wa Aristotle, kuna aina mbili za tamthilia. Aina ya kwanza ni tanzia na nyingine ni ramsa.
  • Tanzia ni nini?

Tuesday 12 November 2013

MOTIFU YA SAFARI


MOTIFU YA SAFARI NA MSAKO KAMA MWEGA MKUU WA DHAMIRA KATIKA “MARIMBA YA MAJALIWA”
“Marimba ya Majaliwa ni hadithi iloyoandikwa na Edwini Semzaba mwaka (2008) ambayo inaelezea kuhusiana na marimba ya Majaliwa iliyopotea. Mwandishi ameonyesha jinsi Majaliwa alivyokuwa anatafuta marimba yake mpaka akaipata. Majaliwa alisafiri kwa kutumia njia mbalimbali kama vile ungo, fagio, na maumbo ya samaki akizunguka Tanzania nzima akisaka marimba ya nyuzi ishirini (20). Alianza Mafia, akaenda Zanzibar, Tanga, Moshi na Arusha, Iringa, Mwanza, Kigoma, na miji mingine mingi. Na Kongoti bingwa wa Taifa wa Marimba akimchenga kila mara huku akinga’nga’nia Marimba ya Majaliwa ili amzuie kushinda na ashinde yeye na bila Marimba yenye nyuzi ishirini (20) hakuna ushindi.

Friday 8 November 2013

SHAIRI


NI WAPI TUMEKOSEA?

Mhadhara nafungua, halaiki karibuni,
Hoja yangu naitoa, kwa makini nyambueni,
Msipandwe na hisia, mkavuruga amani,
Yangu hoja inahoji, NI WAPI TUMEKOSEA?
Tumetenda ndivyo sivyo, kwa kuwaza sivyo ndivyo,
Kwangu mimi ndivyo hivyo, yote nimeona hivyo,
Nanyi wazeni vilivyo, mnene kama ilivyo,
Yangu hoja inahoji, NI WAPI TUMEKOSEA?

TANZU NA VIPERA VYA FASIHI SIMULIZI


VIGEZO ALIVYOVITUMIA MULOKOZI KATIKA KUGAWA TANZU NA VIPERA VYA FASIHI SIMULIZI: KATIKA MULIKA (1989) NAMBA 21
Kwa mujibu wa Mulokozi katika Mulika namba 21(1989). Pamoja na kwamba Fasihi ni kongwe lakini kitaaluma bado ni changa kwa sababu ilianza kuchungunzwa hivi karibuni. Hivyo imepelekea kutokuwepo kwa nadharia, marejeo, wala istilahi zenye kutosheleza mahitaji ya taaluma hiyo. Tatizo hili linadhihirika pale tunapoangalia kazi za wataalamu mbalimbali kuhusu tanzu za Fasihi Simulizi. Kwa upande wa nadharia kitabu pekee kinachozijadili tanzu za Fasihi Simulizi kwa urefu ni kitabu cha Ruth Fennegan kinachoitwa Oral Literature in Africa (1970). Kwa upande wa Kiswahili hakuna kitabu kinachojadili uwanja wa tanzu za Fasihi Simulizi. Badala yake kunamiongozo michache kwa ajili ya shule za sekondari kama vile Balisidya, N (1975) na Taasisi ya Elimu (1987)

Saturday 2 November 2013

FASIHI SIMULIZI



FASIHI SIMULIZI NA MASUALA MTAMBUKO YA KIJAMII BARANI AFRIKA HUSUSANI TANZANIA
Katika kujadili mada hii tutaanza na utangulizi ambao utahusisha maana ya fasihi simulizi kupitia wataalamu mbalimbali, chimbuko la fasihi simulizi kwa kutumia nadharia ya ubadilikaji taratibu na kisha maana ya masuala mtambuko katika jamii. Baada ya hapo kitafuata kiini cha mada yetu, ambapo tutaeleza dhima za fasihi simulizi katika jamii ya leo na namna zinavyohusiana na masuala mtambuko ya kijamii na mwisho kabisa kutakuwa na hitimisho na marejeo.
Fasihisi Simulizi imejadiliwa na wataalam mbalimbali miongoni mwa wataalam hao ni:  M.M. Mulokozi (1996) anasema, Fasihi Simulizi ni fasihi inayotungwa au kubuniwa kichwani na kuwasilishwa kwa hadhira kwa njia ya mdomo na vitendo bila kutumia maandishi.

Friday 1 November 2013

SANAA ZA MAONESHO



SANAA ZA MAONESHO KABLA YA UKOLONI AFRIKA MASHARIKI NA MBINU ZILIZOTUMIKA KUFIFISHA AU KUUA SANAA ZA MAONYESHO HAPA NCHINI

Dhana ya sanaa imejadiliwa na wataalamu mbalimbali, baadhi ya wataalamu hao ni hawa wafuatao
Muhande P, and Balisidya (1976:1). Sanaa ni uzuri unajitokeza katika umbo lililosanifiwa, umbo ambalo mtu hulitumia kueleza hisia zinazomgusa kwa kutoa kielelezo au vielelezo vyenye dhana maalum. Wataalmu hawa wameainisha aina tatu za sanaa ambazo ni sanaa za uonyesho, sanaa za ghibu na sanaa za vitendo
Kwa mujibu wa Mhando na Balisidya (1976) wamekusanya mawazo ya wanazuaoni mbalimbali katika kufasili dhana ya sanaa za maonyesho. Mawazo makuu yaliyotolewa ni kama haya yafuatayo.