Saturday, 29 June 2013

UHAKIKI



Uchambuzi wa tamthiliya ya Sundiata kwa kuzingatia vipengele vya: harmatia, anagnorisisi, hubrisi, nemesisi, na peripeteia. 
Sundiata ni tamthiliya iliyoandikwa na Emmanuel Mbogo na kuchapishwa na TUKI (2011). Ni drama-tanzia inayotokana na dafina ya mapisi ya Afrika Magharibi, lakini ndani ya kioo hiki mwandishi amesanidi na kusawiri mahangaiko na kiwewe cha kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni kinachoendelea kukumba na kukumbatia bara lote la Afrika leo. Katika tamthiliya hii iliyoandikwa kwa ustadi mkubwa tunamwona Sundiata mara tu baada ya kufa baba yake, Maghan Kon Fatta ambaye alikuwa mfalme wa Nianiba Sundiata anadhulumia urithi wake na malkia na kumpatia Dankarani ambaye ni mtoto wake wa kumzaa. Baadaye baada ya mapambano makali Sundiata anafaulu kuchukua ufalme nakuwa mwanasiasa na jemedari shupavu akiongoza majeshi ili kupiga vita udhalimu na uongozi mbovu kama wa akina Sumanguru na hatimaye Sundiata anafaulu kumshinda mfalme Sumanguru, lakini Sundiata hapewi nafasi ya kufurahia ushindi wake na mara baada ya kuupata anapoteza maisha yake kupitia mikono ya mwanamke.
Baada ya kuangalia kwa ufupi historia ya kitabu, ufuatao ni uchambuzi wa tamthiliya ya Sundiata kwa kuzingatia dhana zifuatazo: Harmatia, Peripatea, Anagnorisis, Hubris na Nemesis.

SHAIRI



DAKTARI

Ilikuwa siku moja, mimi na wangu ugonjwa,
Kwenda kwa bwana mmoja, pale mnazi mmoja,
Nilifika na kungoja, tiba ya moja kwa moja,
Tiba hii tiba gani, mbona mimi sifahamu.

Masaa yalipotea, daktari jatokea,
Wasiwasi kunijia, moyo ukinisogea,
Mara kiza kikajaa, sebule kikazagaa,
Tiba hii tiba gani, mbona mimi sifahamu.

Ghafula nilishangaa, kumuona mwenye kaya,
Mrefu aliyejaa, mweupe kama papaya,
Sigara kashikilia, ubani na udi piya
Tiba hii tiba gani, mbona mimi sifahamu.


Friday, 28 June 2013

UHAKIKI



Maisha Yangu na Baada ya Miaka Hamsini.
Kikosi Kazi (Uwasilishaji)

Kitabu cha Maisha Yangu na Baada ya Miaka Hamsini  ni riwaya iliyoandikwa na Shaaban Robert (1936-1946) yenye insha na mashairi yanayoelezea mambo aliyoyafanya kuanzia umri wa ujana mpaka uzee wake, pamoja na mafanikio mbalimbali aliyoyafikia, changamoto alizokumbana nazo na namna alivyozitatua.

DHAMIRI YA MTUNZI
Kwa mujibu ya kamusi ya Karne ya 21(2011) inafafanua kwamba, dhamiri ni ile azma, kusudio au nia ya kufanya jambo. Katika muktadha wa kifasihi tunaweza kusema dhamiri ni lile lengo au kusudi la mtunzi katika kuitunga kazi yake. Na hii inatuthihirishia kwamba, kila mtunzi husukumwa na jambo fulani (ama zito ama jepesi) katika utunzi wake. Hakuna mtunzi anayetunga kazi yake katika ombwe. Mwandishi yoyote yule hata kama anaandika tungo za kubuni, kwa kawaida huwa amesukumwa na jambo au mambo fulani aliyowahi kusikia, kushuhudia katika fikra zake au katika hali halisi maishani; na fikra hizo hujengwa na mambo fulani ya tajiriba halisi katika maisha halisi.

Thursday, 27 June 2013

TASWIRA KATIKA WASAKATONGE



Waandishi wa kazi mbalimbali za kifasihi hutumia taswira kadha wa kadha katika kujenga na kupamba kazi zao.
Fasihi ni kazi ya sanaa itumiayo lugha ili kufikisha ujumbe kwa jamii iliyokusudiwa. Zipo aina mbili za fasihi yaani fasihi andishi na fasihi simulizi. Taswira ni maneno yanayotoa picha ya kitu, hali, wazo au dhana juu ya jambo fulani. Kwa maneno mengine ni lugha ya picha.Taswira humfanya msomaji kuibua hisia na kupata maana akilini mwake juu ya kile kinachosemwa.
Katika Diwani ya Wasakatonge mwandishi Muhammed Seif Khatib ametumia taswira mbalimbali katika kuijenga na kuifanya kazi yake ivutie huku akifikisha ujumbe aliokusudia kwa jamii husika. Mwandishi ametumia taswira zifuatazo;

Sunday, 23 June 2013

KAULI ZETU KATIKA VITENZI




Kauli za vitenzi
TENDA

TENDWA

TENDEWA
TENDEKA
TENDANA

TENDEANA
TENDESHA
Soma

Somwa

Somewa
Someka
Somana

Someana
Somesha
Sema

Semwa

Semewa
Semeka
Semana

Semeana
Semesha
Tema

Temwa

Temewa
Temeka
Temana

Temeana
Temesha
Pita

Pitwa

Pitiwa
Pitika
Pitana

Pitiana
Pitisha
Suka

Sukwa

Sukiwa
Sukika
Sukana

Sukiana
Sukisha
Pata

Patwa

Patiwa
Patika
Patana

Patiana
Patisha
Kimbia

Kimbiwa

Kimbiliwa
Kimbilika
Kimbiana

Kimbiliana
Kimbiza
Tembea

Tembelewa

Tembelewa
Tembeleka
Tembeana

Tembeleana
Tembeza
Paa

Pawa

Paliwa
Palika
Paana

Paliana
Paza
Zaa

Zawa

Zaliwa
Zalika
Zaana

Zaliana
Zalisha
Kaa

Kawa

Kaliwa
Kalika
Kaana

Kaliana
Kalisha
Zoa

-

Zolewa
Zoleka
Zoana

Zoleana
Zolesha
Toa

-

Tolewa
Toleka
Toana

Toleana
Tolesha
Zua

-

Zuliwa
Zulika
-

Zuliana
Zusha
Tia, tua

Tiwa

tuliwa
Tulika,
Tuana

Tuliana
Tulisha
-a-

-w-

-ew-
-liw-
-lew-
-iw-
-ek-
-ik-
-lik-
-lek-
-an-

-ean-
-ian-
-lian-
-lean-

-esh-
-ish-
-z-
-lish-
-lesh-
-sh-

TENDA
TENDWA

TENDEWA

TENDEKA

TENDANA

TENDEANA
TENDESHA

Hakuna alomofu kwa sababu kuna umbo moja

-w-


-ew-
-liw-
-lew-
-iw-




-ek-
-ik-
-lik-
-lek-






-an-



-ean-
-ian-
-lian-
-lean-
-esh-
-ish-
-z-
-lish-
-lesh-
-sh-

-a-
Piga
Suka
Zaa
Soma
sema
-w-
Somwa
Sukwa
Semwa
Zawa
Pitwa






-ew-
Semewa
Temewa
Chekewa
Zolewa
Somewa






-ek-
Semeka
Temeka
Someka
Toleka
zoleka






-an-
Somana
Itana
Toana
Zoana
Patana
Temana
Sukana
Semana









-ean-
Someana
Semeana
Zoleana
Chezeana
Toleana
Temeana
-esh-
Somesha
Semesha
Chezesha
Onesha
Temesha
Zolesha




-iw-
Tiliwa
Pigiwa
Kaliwa
Zaliwa
Tuliwa






-ik-
Pitika
Zalika
Tulika
Kalika
Sukika








-ian-
Zaliana
Tiliana
Zuliana
Patiana
sukiana
-ish-
Pitisha
Pikisha
Limisha
Zalisha
Sukisha




-lew-
Tolewa
Zolewa
Tembelewa




-lik-
Zalika
Kalika
Tulika
Kimbilika
Zulika








-lian-
Zaliana
Kaliana
Kimbiliana
Zuliana
Tiliana
-z-
Tembeza
Kimbiza
Toza
Paza




-liw-
Kaliwa
Tiliwa
Zaliwa
Paliwa
Tuliwa


-lek-
Zoleka
Toleka
Tembeleka




-lean-
Toleana
Zoleana
Tembeleana
-lish-
Kalisha
Tulisha
Zalisha











-lesh
Zolesha
Tolesha
Lelesha











-sh-
Kalisha
Tulisha
Zusha
somesha