Uchambuzi wa tamthiliya ya Sundiata kwa kuzingatia vipengele vya: harmatia, anagnorisisi, hubrisi, nemesisi, na peripeteia.
Sundiata ni tamthiliya iliyoandikwa na Emmanuel Mbogo na kuchapishwa na TUKI (2011). Ni drama-tanzia inayotokana na dafina ya mapisi ya Afrika Magharibi, lakini ndani ya kioo hiki mwandishi amesanidi na kusawiri mahangaiko na kiwewe cha kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni kinachoendelea kukumba na kukumbatia bara lote la Afrika leo. Katika tamthiliya hii iliyoandikwa kwa ustadi mkubwa tunamwona Sundiata mara tu baada ya kufa baba yake, Maghan Kon Fatta ambaye alikuwa mfalme wa Nianiba Sundiata anadhulumia urithi wake na malkia na kumpatia Dankarani ambaye ni mtoto wake wa kumzaa. Baadaye baada ya mapambano makali Sundiata anafaulu kuchukua ufalme nakuwa mwanasiasa na jemedari shupavu akiongoza majeshi ili kupiga vita udhalimu na uongozi mbovu kama wa akina Sumanguru na hatimaye Sundiata anafaulu kumshinda mfalme Sumanguru, lakini Sundiata hapewi nafasi ya kufurahia ushindi wake na mara baada ya kuupata anapoteza maisha yake kupitia mikono ya mwanamke.
Baada ya kuangalia kwa ufupi historia ya kitabu, ufuatao ni uchambuzi wa tamthiliya ya Sundiata kwa kuzingatia dhana zifuatazo: Harmatia, Peripatea, Anagnorisis, Hubris na Nemesis.